• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
SONGWE REGION
SONGWE REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MKOA WA SONGWE

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Sehemu
      • Mipango na Uratibu
      • Idara ya Elimu
      • Huduma za Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
  • Wilaya
    • Mbozi DC
    • Songwe DC
    • Momba DC
    • Ileje DC
  • Halmashauri
    • Mbozi
    • Ileje
    • Momba
    • Songwe
    • Tunduma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Mifugo
    • Madini
    • Kilimo
    • Biashara
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya na Ustawi Wa Jamii
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma ya Mifugo na Uvuvi
    • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
    • Mipango na Takwimu
    • Ujenzi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Utaratibu
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA SONGWE MHE. DKT FRANCIS K. MICHAEL AMETATUA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU ZAIDI YA MIAKA 19.

Posted on: October 10th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Dkt. Francis K. Michael, amefanikiwa kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 19 baina ya kijiji cha Nanyala na kiwanda cha Saruji cha Mbeya. Hatua hii ya kutatua mgogoro huu imesababisha kutoa suluhisho la kihistoria kwa pande zote husika.

Dkt. Francis, aliwaita pande zote za mgogoro wa ardhi, yaani Kiwanda cha Saruji cha Mbeya na Wanakijiji cha Nanyala, na kuwataka kiwanda cha Saruji cha Mbeya kutoa eneo la hekari 62.5 kutoka kwenye ardhi yao ili kuwapatia wachimbaji wadogo wanaotoka katika kijiji cha Nanyala.

Mbali na kutoa eneo hilo kwa wachimbaji lakini pia kiwanda cha saruji mbeya kimekubali ombi la mkuu wa mkoa kutowafukuza wananchi wanaofanya Shughuli za kilimo na ufugaji katika eneo la kiwanda na badalayake wawaache waendelee kufanya shughuri hizo kwa mikataba ya mwaka mmoja mmoja.

Dkt. Francis alitoa hati miliki ya maeneo kwa wanakijiji wa Nanyala na wamiliki wa kiwanda cha Saruji kilicho mpakani mwa mikoa ya Mbeya na Songwe. amedhihirisha uongozi wake wa kipekee katika kutatua migogoro na kuleta maendeleo kwa wananchi wa mkoa huo. Amesisitiza umuhimu wa amani na ushirikiano katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika eneo hilo.

Akizungumza, Dkt. Francis alisema, "Nimeteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kutatua changamoto za wananchi. Tunaamini kuwa amani ni msingi wa maendeleo, na leo tumeweza kurejesha amani na furaha kwa wananchi wa kijiji cha Nanyala."

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Esther Mahawe, pia amepongeza juhudi za kila mtu aliyejitolea katika mchakato huu wa kutatua mgogoro huo. Amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuleta maendeleo na amani kwa kijiji cha Nanyala.

Wananchi wametoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa, Dkt. Francis kwa kazi yake nzuri katika kuwezesha kutatuliwa kwa mgogoro huo wa ardhi, na kwa kuweka msingi wa maendeleo na amani katika eneo la Songwe. Zawadi ya mbuzi ili tolewa na wananchi ikiwa ni ishara ya ukarimu wa wananchi wa eneo hilo na shukrani kwa uongozi wake wa ujasiri na hekima kubwa katika kutatua migogoro kwa amani.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI January 30, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YA SAINI MRADI WA ZAIDI YA BILIONI 119.9 UJENZI WA MRADI WA MAJI TUNDUMA VWAWA

    March 20, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE MHE. FARIDA MGOMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA AFUNGUA HUDUMA YA WIKI YA SHERIA MKOANI SONGWE

    January 25, 2025
  • TASAF MKOA WA SONGWE IMEFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI NA KUJIONEA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANUFAIKA WA TASAF MOMBA

    January 03, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO MKOANI SONGWE.

    November 07, 2024
  • Angalia zote

Video

ELIMU KWA WATOTO KIPINDI CHA CORONA
Video za Ziada

Kurasa za Karibu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • SALARY SLIP PORTAL
  • AJIRA

Kurasa Mashuhuri

  • IKULU
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    2 Nselewa Mkoani RD, 54180 Mlowo-Mbozi

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 23 SONGWE

    Simu: 025 2580305

    Simu ya Kiganjani: 025 2580305

    Barua pepe: ras@songwe.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki©2020 Mkoa wa Songwe.Haki Zote Zimehifadhiwa.